ZIARA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI KATIKA VISIMA VYA GESI ASILIA, MADIMBA


Picha Na 1
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Evodi Mmanda (mbele) akizungumza na  wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, kabla ya kuanza kwa ziara katika miradi mbalimbali ya gesi asilia iliyopo mkoani humo.
Picha Na 2
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia (kulia) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto mbele) wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na  Meneja wa Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Madimba kilichopo Mtwara, Leonce Mroso (hayupo pichani) kwenye  eneo la kiwanda hicho katika ziara hiyo. Katikati nyuma ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Jaji Mstaafu, Josephat Mackanja.
Picha Na 3
Sehemu ya mitambo ya Kiwanda cha Kuchakata Gesi cha Mnazi Bay kilichopo mkoani Mtwara
Picha Na 4
Mtaalam kutoka Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Mnazi Bay kilichopo mkoani Mtwara, Laurent Jars (katikati) akielezea shughuli za uchakataji wa gesi zinavyofanywa na kiwanda hicho kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti.
  Picha Na 5
Mtaalam kutoka Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Mnazi Bay kilichopo mkoani Mtwara, Nyomwa Kilemo (katikati) akifafanua jambo kwa  wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwenye ziara hiyo.
Picha Na 6
Mtaalam kutoka Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Mnazi Bay kilichopo mkoani Mtwara, Laurent Jars (kulia) akifafanua jambo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto) kwenye ziara hiyo.
Picha Na 7
Mtaalam kutoka Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Mnazi Bay kilichopo mkoani Mtwara, Laurent Jars (kushoto) akielezea usafirishaji wa gesi asilia kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia (kulia) katika ziara hiyo.
Picha Na 8
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia (katikati) akionesha wajumbe wa kamati hiyo  sehemu ya eneo la Pwani lililomegwa na maji karibu na Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Mnazi Bay kilichopo mkoani Mtwara kwenye ziara hiyo.
Picha Na 9
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia (kulia mbele) akielezea manufaa ya gesi asilia kwenye uchumi wa mkoa wa Mtwara kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwenye ziara hiyo.
Picha Na 10
Sehemu ya mitambo ya Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Madimba  kilichopo mkoani Mtwara.
Picha Na 11
Meneja wa Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Madimba kilichopo Mtwara, Leonce Mroso (kulia) akielezea matumizi ya  gesi asilia kwenye uzalishaji wa umeme kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwenye eneo la kiwanda hicho.
Picha Na 12
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia (wa tatu kulia mbele) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo ( wa pili kulia mbele) wakiongoza wajumbe wa kamati hiyo kwenye ziara katika eneo la Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Madimba kilichopo mkoani Mtwara.
……………………..
Wataalam Madimba watakiwa kuwa wazalendo
Na Greyson Mwase, Mtwara
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia amewataka  vijana wanaofanya kazi katika Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Madimba kilichopo mkoani Mtwara kuwa wazalendo na kufanya kazi kwa weledi, hivyo kuwa na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi kupitia sekta ya gesi.
Ghasia aliyasema hayo kwenye ziara ya kamati hiyo kwenye miradi mbalimbali ya  gesi mkoani Mtwara yenye lengo la kujionea mafanikio na changamoto zake.
Alisema Serikali imekuwa ikisomesha vijana katika  masuala ya gesi na mafuta, ndani na nje ya nchi lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa vijana wanakuwa sehemu  ya umiliki wa  uchumi wa gesi asilia.
Aidha, katika hatua nyingine, alishauri  Shirika la Maendeleo ya Petroli  Tanzania (TPDC) kuendelea na mikakati ya kuwa programu za mafunzo ya mara kwa mara kwa wataalam hao kwa kuwa teknolojia inabadilika kila wakati.
“ Vijana wanaofanya kazi nzuri katika kiwanda hiki ni vyema wakahudhuria mafunzo ya mara kwa mara ili kuendana na teknolojia inayobadilika mara kwa mara.
Pia alishauri maslahi kwa ajili ya vijana wanaofanya kazi katika kiwanda hicho yakaendelea kuboreshwa zaidi ili kuwapa motisha wa kazi zaidi.

Mhe. Mahiga Ampokea Waziri wa Nchi wa Uingereza Ambaye Yupo Ziarani Nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Waziri wa Nchi anayeshughulikia masuala ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza, Mhe. Stewart Rory alipofika Wizarani tarehe 22 Agosti, 2017 kwa ajili ya mazungumzo rasmi na Waziri Mahiga. Katika mazungumzo yao walisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Uingereza. Serikali ya Uingereza kupitia Shirika lale la Kimataifa la Maendeleo (DFID) inaisadia Tanzania katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Maji, Elimu, Nishati Mbadala na mapambano dhidi ya madawa ya kulevya. Mhe. Stewart yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili tarehe 22 na 23 Agosti, 2017
.
Sehemu ya ujumbe ulioambatana na Mhe. Stewart. Kulia ni Balozi wa Uingereza hapa nchini, Mhe. Sarah Cooke, Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Uingereza (DFID), Bi. Beth Arthy na Afisa kutoka Ubalozini.
Sehemu ya ujumbe wa Wizara wakati wa mazungumzo kati ya Waziri Mahiga na Waziri Stewart kutoka Uingereza (hawapo pichani). Kushoto ni Bw. Salvatory Mbilinyi, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Mindi Kasiga, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Bw. Joseph Kapinga, Afisa Mambo ya Nje.
Waziri Mahiga akiagana na mgeni wake Mhe. Stewart mara baada ya kumaliza mazungumzo yao
Picha ya pamoja
Waziri Mahiga kwa pamoja na Mhe. Stewart wakizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu lengo la ziara ya Mhe. Stewart nchini.
Mkutano na waandishi wa habari ukiendelea

zanzibariyetu, Zanzibar Yetu just now


Waahidiwa kiwanja cha kimataifa

Dk. Ali Mohamed Shein, amewaahidi wananchi wa Kitogani kuwa uwanja wao utatengenezwa kwa kiwango ha Kimataifa kitakachoshirikisha michezo ya aina mbali mbali.

Dk. Shein aliwaeleza wananchi hao wa kijiji cha Kitogani kuwa kijiji chao kitakuwa eneo la michezo kwani watafika watu kutoka ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kuutumia uwanja wao mpya unaoendelea kujengwa ambao tayari kwa awamu ya kwanza umekamilika.

Hivyo, amewataka wakaazi wa Kitogani kujiandaa kuwapokea wageni wakiwemo wanamichezo huku akieleza jinsi Serikali ilovyojiandaa kukijenga kiwanja hicho kuwa cha kisasa na kuweza kuchezwa michezo kadhaa mbali na mpira wa miguu.

KISHAPU YAZINDUA KAMPENI YA KUHAMASISHA WANANCHI KATIKA SHUGHULI ZA KILIMO NA ELIMU


 

3

Katibu Tawala wa Wilaya, Shadrack Kengese akizungumza na wananchi wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha shughuli za kilimo na elimu kwa wananchi. Ofisa Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika katika halmashauri ya wilaya ya Kishapu, Godwin Everygist akifafanua jambo kwa wananchi wakati wa uhamasishaji wa shughuli za kilimo. Ofisa Elimu Sekondari …

Read More »

WAZIRI WA ELIMU PROF. NDALICHAKO AZINDUA BODI MPYA YA MAMLAKA YA ELIMU TANZANIA (TEA)


1

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako (kulia) akielekea kwenye ukumbi kwaajili ya kuzindua Bodi mpya ya Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) leo jijini Dar es Salaam (kushoto) Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA ) Graceana Shirima .

2

Wajumbe wa Bodi ya Elimu Tanzania (TEA) wakiwa wamejipanga kumpokea mgeni rasmi Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako wakati wa uzinduzi wa Bodi mpya ya Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) leo jijini Dar es Salaam.

HEBU CHEKI….WANANCHI WAPONGEZA UKAMILISHAJI WA BARABARA MKOANI RUVUMA


1

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akisikiliza maoni kutoka kwa Bw. Mohammed Ally mkazi wa Nakapanya, Wilayani Tunduru, Mkoani Ruvuma kuhusu furaha yao juu ya kukamilika kwa ujenzi wa Barabara ya Nakapanya-Tunduru KM 66.5.

2

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akionesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani), picha ya barabara ya Nakapanya-Tunduru KM 66.5 iliyokamilika kwa kiwango cha lami wakati alipokuwa akikagua barabara hiyo, mkoani Ruvuma. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Bw. Juma Homera.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza na wadau wa sekta ya filamu…


NAP1

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kushoto) akizungumza na wadau wa sekta ya filamu (hawapo pichani) wakati wa kikao cha wadau kuzungumzia sera ya filamu leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Naibu Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura na Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bibi. Nuru Millao