Mkuu
wa masoko na mawasiliano wa benki ya NBC Mwinda Kiula Mfugale (kushoto)
akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma ya master card ya benki ya NBC
jijini Dar jana.katikati ni mkuu wa kitengo cha shughuli za kibenki wa
benki hiyo William Kalaghe, na kulia ni meneja wa card
wa NBC Robert Mng"hanya.
Meneja wa Card Ndg Robert Mngh"anya akitoa ufafanuzi juu ya matumizi ya Card hiyo mpya
NA DANIE SEMBERYA
Benki
ya Taifa ya Biashara (NBC) moja ya benki kongwe sana nchini leo
imezindua kadi ya mastercard ikiwa ni moja ya juhudi za makusuidi
zinazofanywa na benki hiyo katika kuhakikisha wateja wake wanapata
huduma bora mahali popte walipo nchini na duniani kote.
Kwa
mjibu wa mkuu wa kitengo cha masoko na mawasiliano wa benki ya NBC Bi.
Mwinda Mfugale, mteja wa NBC sasa anaweza kupata huduma za kibenki
katika mashine yoyote ya kutolea fedha (ATM) inayokubali mfumo wa
MasterCard.
Mfugale
ameongeza kuwa wateja wa benki ya NBC wanweza pia kufurahia na kuwa na
amani kwani kwa kupitia kadi ya MasterCard unakuwa na uhakika kutoa
fedha, kufanya manunuzi au kupitia huduma mbalimbali kwa kupitia mfumo
huo mahali popote pale duniani.
“Ili
kuhakikisha mteja wa NBC anafurahia na kuridhishwa na kadi yake mpya ya
MasterCard, NBC tumefanya utafiti wa muda mrefu ilikuhakikisha tunakuja
na kadi itakayokidhi mahitaji ya wateja wetu katika soko la fedha
kitaifa na kimataifa,” amesema Bi. Mfugale.
Na
kwa wateja wao wa zamani wanaotumia kadi zilizopo utaratibu
umeshandaliwa ambapo mteja huyo akifika katika tawi lolote la benki ya
NBC anapwe fomu ya kujaza na kasha kupewa kadi yake ya MasterCard kwa
muda mfupi zaidi wakati wale wateja wapya watapaswa kufuata taratibu za
kawaida za kibenki za NBC ilikufungua akaunti na kupewa kadi hiyo.
“Kuwa
na kadi ya banki ni kitu kimoja , bali kuwa na uhakika wa kupata huduma
bora isiyo na usumbufu kupitia kadi hiyo ni kitu kingine na ndio maana
sisi katika NBC tukaona hatuna budi kuchukua muda wa kutosha kujipanga
vizuri katika kila eneo ili mteja wetu aweze kufurahia huduma bora
kupitia kadi yake ya mastercard ya benki iliyo karibu nawe kila mahali
yaani benki ya NBC,’Bi. Mfugale ameongeza.
Naye
mkuu wa kitengo cha shughuli za kibenki katika benki ya NBC Bw. William
Kallaghe alisema “NBC imeamua kuzindua huduma hii kwa wakati huu baada
ya kufanya uhakiki wa uslama wa hali ya juu ilikufikia viwango vya ubora
vya kibenki na kimataifa,”. Na kuongeza kuwa huduma hii inapatikana kwa
wateja wetu wapya baada ya kukamilisha utaratibu wa kufungua akaunti,
na kwa wateja wetu wa zamani baada ya kujaza fomu za kubadili kadi zao
za zamani watapata mpya,” alisemaKallaghe.
Kallaghe
amewahakikishia wateja “Ningependa kuwahakikishia wateja wetu kuwa bei
zetu za huduma ziko palepale na hamna mabadiliko yoyote kwa kipindi
hiki,” Kallaghe alijisifu.
Kallaghe
amewaomba wateja kujivunia huduma hii kwani kwani kadi hizi hupatikana
papo kwa papo, tofauti na utaratibu wa zamani wa kusubiria kadi, kitu
ambacho benki ya NBC imekuwa ya kwanza kuzindua.
NBC
iliundwa Mwezi April, 2000 baada ya ubinafsishwaji na kuuzwa kwa benki
ya ABSA ya Afrika Kusini inayomiliki Hisa asilimia 55 huku serikali ya
Tanzania ikimiliki Hisa 30 na zinazobaki asilimia 15 zikimilikiwa na
mashirika ya kifedha ya kimataifa.
NBC inamtandao wa matawi 54 nchini kote na mashine za kutolea fedha zaidi ya 250.
1 comment:
2gether we are saying thanks very much about your services(MasterCard) but on the other hand those improvement of technology are the among of the techniques of FREE MASONS to attract people in their culture(beliefs). Few people understand this issue....But am sorry!! Thanks 4 MasterCard,it is good,better & best 4 us.
Post a Comment