Wednesday, June 19, 2013

HEBU CHEKI JINSI LULU ANAVYOPIGA 'BATA '...!

Ni Lulu Semagongo aka lulu Kimwana akiwa ndani ya ukumbi wa Mango Garden maeneo ya Kinondoni  huku African Stars wakitoa burudani kwa kwenda mbele! Pia unaweza kubonyeza...http://Wwwmasterkif.blogspot.com

DIAMOND : PREZZO KWANGU HANA LOLOTE


Diamond akilonga na Sauda kuhusu shoo kali atakayotoa Usiku wa Matumaini 2013.
Sauda na Diamond wakiwa mbele ya kamera.
Platnumz akijiaandaa kabla ya mahojiano.
...Akibadilishana mawazo na Sauda kabla ya kuanza mahojiano.
Mtu wa kamera akiwa mzigoni.Chanzo:www.globalpublishers.info

Peroni Jazz Sundays


Kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu:Waziri Mkuu Mizengo Pinda Amjulia Hali Wabunge wa Chadema Mbunge wa Arumeru Mashariki-Chadema , Joshua Nasari ambaye amelazwa katika hospitali ya Serian Arusha anakotibiwa kwa madai ya kushambuliwa na wananchi eneo la Makuyuni na Mbunge wa Viti Maalum, Namelok Sokoinine aliyelazwa kwenye hospitali ya Serian Arusha baada ya kuvunjika mguu akiwa nyumbani kwake.


 Waziri mkuu, Mizengo Pinda akimpa pole mbunge wa Arumeru Mashariki-Chadema , Joshua Nasari ambaye amelazwa katika hospitali ya Serian Arusha anakotibiwa kwa madai ya kushambuliwa na wananchi eneo la Makuyuni.
Waziri mkuu, Mizengo Pinda akimpa pole Mbunge wa Viti Maalum, Namelok Sokoinine aliyelazwa kwenye hospitali ya Serian Arusha baada ya kuvunjika mguu akiwa nyumbani kwake.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

OMMY DIMPOZ AOMBA MSAMAHA


Na Mwandishi Wetu

KUFUATIA kumtusi marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ kuwa amekufa maskini, mmiliki wa akaunti inayodaiwa ni ya msanii Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ katika mtandao wa Facebook, amewaomba msamaha Watanzania kwa kitendo chake hicho baada ya kumwagiwa mitusi.
Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’.
Katika akaunti hiyo yenye jina la Ommy Dimpoz- Omary Faraji, mwishoni mwa wiki iliyopita ilijaa matusi na maneno makali yakimnanga jamaa huyo kwa kauli yake aliyoitoa hivi karibuni kwenye Tuzo za…
Na Mwandishi Wetu
KUFUATIA kumtusi marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ kuwa amekufa maskini, mmiliki wa akaunti inayodaiwa ni ya msanii Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ katika mtandao wa Facebook, amewaomba msamaha Watanzania kwa kitendo chake hicho baada ya kumwagiwa mitusi.
Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’.
Katika akaunti hiyo yenye jina la Ommy Dimpoz- Omary Faraji, mwishoni mwa wiki iliyopita ilijaa matusi na maneno makali yakimnanga jamaa huyo kwa kauli yake aliyoitoa hivi karibuni kwenye Tuzo za Kili.
Aliandika: “Binadamu ni kukosea mara nyingi na-regret (kujuta) kwa yale niliyosema kuhusu Ngwea. Kama ningekuwa na uwezo wa kurudisha siku na maneno nyuma, yale ndo yangekuwa ya kwanza.
“Nakubali nilifanya kosa kubwa sana na nikaweka pride (majivuno) yangu na sifa zangu mbele bila kufikiria nitakayosema.
“Nyumbani Tanzania, Bongo nimeenda hadi kwa redio stations kuwaomba msamaha.
Albert Mangweha ‘Ngwea’.
“Team Kigoma All Stars na wasanii wenzangu wa Bongo, Kenya, Uganda na nchi nyingine zote nisameheni tafadhali.
“I have learnt to think about what I say before I Talk or let it out of my mouth (Nimejifunza kufikiri chakusema kabla ya kukizungumza au kukiacha kitoke mdomoni mwangu).
“Nimewakosea familia ya Ngwea na ma-fans (mashabiki) wangu wanaonipenda hata pia kwa Allah Mungu Baba, naombeni msamaha tafadhali.”
Pamoja na kuomba msamaha bado watu waliendelea kumponda wakihoji ni kitu gani Ngwea alimfanyia huku mwanamuziki Khaleed Mohamed ‘TID Mnyama’ akiahidi kumpa kichapo.Baada ya kuomba msamaha, msanii huyo anayechipukia alidaiwa kupanga safari ya kwenda Morogoro kuiomba msamaha familia ya Ngwea.Chanzo:www.globalpublishers.info

YAYA TOURE ANALIPWA MILIONI 400 KWA WIKI(FEDHA YA KITANZANIA)


 
Yaya Toure 
Unaweza kusema kuwa leo King kif nafanya utani!Jamani ni kweli mchezaji huyu analipwa kiasi hicho cha pesa.wiki iliyopita wakati Taifa stars ilipocheza na Ivory Coast , mchezaji huyu alikuwa makini na hakuwa na pupa kabisa uwanjani.Mara nyingi ukimuona mchezaji anafanya hivyo , bas tambua kuwa anauwezo mkubwa wa kucheza mpira.
Pia unaweza kubonyeza...http://Wwwmasterkif.blogspot.com  

Arfi, Lissu watiwa mbaroni Arusha

Arusha. Wabunge wanne wa Chadema, Said Arfi (Mpanda Mjini), Tundu Lissu (Singida Mashariki), Mustapha Akunaay (Mbulu) na Joyce Mukya (Viti Maalumu) wamekamatwa wakituhumiwa kuhusika na mkusanyiko usio halali kwenye Uwanja wa Soweto jana.
Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja alisema jana kwamba pamoja na wabunge hao pia wamewakamata watu wapatao 60 kutokana na vurugu zilizozuka jana baada ya Polisi kuwatawanya kwenye uwanja huo waliokuwa wamekusanyika kuomboleza vifo vya watu watatu; 
Judith Moshi, Ramadhan Juma na Amir Ally waliofariki kwenye mlipuko wa bomu uliotokea kwenye uwanja huohuo, Jumamosi iliyopita.
Mbali ya viongozi hao, alisema wanawasaka Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.
“Tunawasaka wabunge ili tuwajumuishe na watu hawa kwa kosa la kuhusika na mkusanyiko usiokuwa halali. Hadi sasa tumefanikiwa kulinasa gari la Mbowe,” alisema Chagonja.
Pia kamatakamata hiyo imemkumba Mpigapicha wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Ashraf Bakari. Polisi walilazimika kutumia nguvu kuwatawanya waombolezaji hao.
Awali, Kamishna Chagonja alisema jana asubuhi kuwa wamelazimika kuzuia viwanja hivyo kutumika baada ya wamiliki wake, AICC kuzuia shughuli za Chadema kwenye eneo lao.
Kamishna Chagonja aliwaonyesha waandishi wa habari barua aliyosema imeandikwa na uongozi wa AICC kuzua Chadema kuendelea kuutumia Uwanja wa Soweto.
Mabomu yarindima
Dalili za kuzuka kwa vurugu zilianza kuonekana asubuhi baada ya polisi kuzingira uwanja huo na kuzuia watu waliokuwa wameanza kufurika katika eneo hilo kuanzia saa moja kuingia kwa ajili ya maombolezo.

GERALD HANDO NUSURA AUAWE


Na Sifae Paul
MTANGAZAJI  mwenye jina kubwa wa Radio Clouds FM, Gerald Hando ‘Mzee Mnoko’  ameponea chupuchupu kuuawa baada ya kutishiwa kwa bastola.
Kwa mujibu wa chanzo makini, tukio hilo lilijiri maeneo ya Mwananyamala Kwa Kopa, Dar alfajiri ya Jumatatu wiki hii.

Ilikuwaje?
Baada ya kutonywa mkasa huo, gazeti hili liliwasiliana na Hando ambaye siku hiyo alishindwa kutokea kwenye kipindi chake cha Power Breakfast na  alielezea kisa kizima.
Alisema: “Ilikuwa saa 12:40 wakati nakatiza pale Kwa Kopa, kabla sijaingia barabara ya kuelekea Ali Hassan Mwinyi, ghafla lilitokea gari aina ya RAV4. Lilikuwa limebana sana upande wangu, ghafla nikasikia kama limenigonga, niliposhusha kioo, kweli nikaona gari langu limegongwa.
“Nilichungulia kwenye lile gari nikamuuliza dereva kwa ishara vipi?
“Nilipoona hanijibu nilifunga vioo vya gari langu nikawa nimetulia,  nikapigwa na butwaa kumuona yule jamaa ameshuka akiwa na bastola.
“Alinigongea kioo lakini sikufungua, nilikuwa nimetaharuki sielewi nini kinaendelea. Lakini wakati ananitishia kuwa nishuke anipige, kuna mwanamke alikuwa naye kwenye gari lake ambaye alishuka na kumlazimisha warudi kwenye gari lao.
“Akiwa ndani ya gari lake, jamaa alifyatua risasi iliyovunja kioo cha mbele cha gari lake na sijui risasi ilielekea wapi maana nilikuwa nimeshachanganyikiwa.
“Kama hiyo haitoshi, jamaa alishuka kwa mara nyingine akiwa na hasira sana na kunifuata tena akitaka kunifyatulia risasi, alipoona imeshindikana alipasua tairi za kushoto za gari langu huku akiniambia ndiyo mchezo umeanza nitaona.
“Bahati nzuri polisi walishafika eneo la tukio kwa sababu ishu yenyewe ilichukua muda mrefu, tulichukuliwa wote hadi Oysterbay (kituo cha polisi) nikatoa maelezo yangu na kumfungulia jalada la kesi namba OB/RB/10613/13 (SHAMBULIO),” alisimulia Hando.
Hadi tunakwenda mitamboni sakata hilo halikujulikana hatma yake, tunaahidi kuendelea kulifuatilia.
Chanzo:www.globalpublishers.info

Tanzania set to reap from Obama’s visit

By CHABY BARASA
Tanzania has said it will capitalise on the forthcoming visit by United States President Barack Obama to promote bilateral ties between the two countries.
President Jakaya Kikwete
President Jakaya Kikwete
President Jakaya Kikwete said the US has been one of his country’s important development partners and noted that the visit ‘’would further cement the existing good ties.’’
“The US is our long time ally. We have important programmes in areas like infrastructure and health under the MCC and PEPFAR which have been a huge success so far,” said Mr Kikwete when fielding questions from the media here on Sunday.
Under the Millennium Challenge Corporation, Tanzania and USA signed a compact agreement for the 698 million US dollar-grant, for a period of five year in 2008. The money was meant to help fund infrastructure projects in line with Tanzania’s poverty alleviation initiatives.
Through the US President’s Emergency Plan for AIDS Relief, Tanzania has received 1076.4 million US dollars to support comprehensive HIV/AIDS prevention, treatment and care programmes from 2009 to 2011.

International Sickle Cell Day Campaign


19th June marks World Sickle Cell Day. Please support the initiative by posting or making this your profile picture on your Facebook page.

Pia unaweza kuingia ...http://Wwwmasterkif.blogspot.com

Tuesday, June 18, 2013

VODACOM YAPANUA WIGO HUDUMA NA AJIRA KWA WATANZANIA


Mkuu wa Idara ya Mauzo na Maduka wa Vodacom Tanzania, Bi. Upendo Richard (kulia) akimkabidhi funguo  Meneja wa duka jipya la Vodacom lililopo Millennium Tower ghorofa ya kwanza Bi. Miriam Minja, ikiwa ni inshara ya uzinduzi rasmi wa duka hilo. Anayeshuhudia ni Mkuu wa kitengo cha Mahusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi.Joseline Kamuhanda.
Meneja wa duka jipya la Vodacom lililopo Millennium Tower ghorofa ya kwanza Bi. Miriam Minja, akifungua duka hilo kwa mara ya kwanza tayari kwa kutoa huduma kwa wateja wa kampuni hiyo, akishuhudiwa na Mkuu wa Idara ya Mauzo na Maduka wa Vodacom Tanzania, Bi. Upendo Richard (kulia) na Mkuu wa kitengo cha Mahusiano ya jamii na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Joseline Kamuhanda.
Mkuu wa kitengo cha Mahusiano ya jamii na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bi. Joseline Kamuhanda, akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa duka jipya la kampuni hiyo lililopo Millennium Tower ghorofa ya kwanza.
Meneja wa duka jipya la Vodacom lililopo Millennium Tower ghorofa ya kwanza, Bi. Miriam Minja (kulia), akimuonyesha mojawapo ya simu zinazopatikana dukani hapo mteja Lameck Hanold (katikati). Anayeshuhudia ni Mkuu wa Idara ya Mauzo na Maduka wa Vodacom Tanzania, Bi. Upendo Richard (kushoto).
---
•           Watanzania zaidi kuendelea kupata huduma za mawasiliano
Dar Es Salaam, June 18, 2013 … Huku jiji la Dar es Salaam likiendelea kukua kwa kasi na kushuhudia ongezeko kubwa la watu kutoka sehemu mbalimbali, upatikanaji wa huduma mbalimbali za kijamii umekuwa ukikabiliwa na changamoto kadhaa kutokana na kasi ya utoaji huduma kutoendana na kasi ya ongezeko la watu.
Katika kukidhi haja hiyo ya utoaji wa huduma kwa wateja na elimu kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam, Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania imeendelea kupanua wigo wa ajira na huduma kwa kufungua duka la huduma kwa wateja katika jengo la Milenium Tower lililoko Makumbusho jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia wakati wa uzinduzi wa duka hilo, Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Joseline Kamuhanda, amesema Vodacom ni kampuni pekee ambayo imeendelea kuongoza kwa kuwa na maduka mengi ya mauzo na huduma kwa wateja kwa kufikisha maduka 66 ikiwa ni kampuni pekee kuwa na maduka mengi ya huduma na kufanikisha adhma ya kukidhi mahitaji ya huduma kwa wateja wa kampuni hiyo, huku Dar es Salaam ikiwa na idadi ya maduka 21.
“Ukuaji wa huduma kwa kampuni ya Vodacom umekuwa kwa kasi, huduma kama ya M – Pesa sasa imepanuka kwa kasi na kutoa huduma kwa watanzania zaidi ya milioni 10. Kufuatia mafaanikio haya tunalazimika kuhakikisha upatikanaji wa huduma kwa wateja  ni wa uhakika” alisema Kamuhanda na kuongeza kuwa,
“Kuongoza katika sekta ya mawasilaino kuna changamoto zake, lazima tuhakikishe tunaendana na kasi ya ukuaji na ongezeko la watu na uhitaji wa huduma zetu kwa watu wa aina mbalimbali.
Aidha Kamuhanda alisema kuwa Kufunguliwa kwa duka hilo sasa sio tu kunaboresha upatikanaji wa huduma pia ni fursa pekee ya kuendelea kupanua wigo wa ajira kwa watanzania.
“Ufunguzi wa duka hili unatoa fursa ya ajira kwa watanzania, ambapo wafanyakazi wapatao 3 watatoa huduma kwa wateja wetu hivyo ni hatua kubwa kwa kutengeneza ajira kwa wafanyakazi wapya. Hadi kufikia sasa, Vodacom imetoa ajira za moja kwa moja kwa wafanyakazi 500 na wengine zaidi ya 450,000 wenye ajira zisizo rasmi,” alisema Kamuhanda.

Tanzania na Japan zimetiliana saini mkataba wa makubaliano wa mkopo wenye riba nafuu wa kuikopesha Tanzania shilingi bilioni 77.7 kwa ajili ya kutekeleza shughuli za maendeleo hapa nchini Pamoja na ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini


Waziri wa Fedha Dkt .William Mgimwa (katikati ) na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la  Japan hapa nchini(JICA) Yasunori Onishi(kulia)wakisaini  hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu ambapo Japan itaikopesha Tanzania shilingi  bilioni 77.7 kwa ajili ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini. Sherehe zilifanyika jana (leo) mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli(kushoto)
 Waziri wa Fedha Dkt .William Mgimwa (katikati ) na Balozi wa Japan nchini Masaki Okada(kulia)wakisaini  hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu ambapo Japan itaikopesha Tanzania shilingi  bilioni 77.7 kwa ajili ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini. Sherehe zilifanyika jana (leo) mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli(kushoto)
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la  Japan hapa nchini(JICA) Yasunori Onishi(kulia) na Waziri wa Fedha wakibadilishana hati ya ujenzi wa  daraja la juu katika makutano ya TAZARAjana(leo) mjini Dodoma wakati wa sherehe za kusaini hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu ambapo Japan itaikopesha Tanzania shilingi  bilioni 77.7 kwa ajili ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini. Wengine ni Balozi wa Japan nchini Masaki Okada ( kulia) ,  na  Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli(katikati)
 Waziri wa Fedha Dkt .William Mgimwa (kushoto) na Balozi wa Japan nchini Masaki Okada(kulia)wakibadilishana hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu ambapo Japan itaikopesha Tanzania shilingi  bilioni 77.7 kwa ajili ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini. Sherehe zilifanyika jana (leo) mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli(katikati) 
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la  Japan hapa nchini(JICA) Yasunori Onishi(kulia) akielezea mkakati  watakaoutumia katika ujenzi wa daraja la juu katika makutano ya TAZARAjana(leo) mjini Dodoma wakati wa sherehe za kusaini hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu ambapo Japan itaikopesha Tanzania shilingi  bilioni 77.7  kwa ajili ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini. Wengine ni Balozi wa Japan nchini Masaki Okada ( wa pili kutoka kulia) , Waziri wa Fedha Dkt William Mgimwa (wa pili kushoto)  na  Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli(kushoto)
 Balozi wa Japan nchini Masaki Okada(kulia) akizungumza na waandishi wa habari jana (leo) mjini Dodoma mara baada yake kusaini na Tanzania hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu ambapo Japan itaikopesha Tanzania shilingi  bilioni 77.7 kwa ajili ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini. Wengine ni Waziri wa Fedha Dkt .William Mgimwa (katikati) na  Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli(kushoto)
 Waziri wa Fedha Dkt .William Mgimwa (kushoto) na Balozi wa Japan nchini Masaki Okada(kulia)wakibadilishana hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu ambapo Japan itaikopesha Tanzania shilingi  bilioni 77.7 kwa ajili ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini. Sherehe zilifanyika jana (leo) mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli(katikati)
Dr. Magufuli—Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli(kushoto) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari jana(leo)  mjini Dodoma juuu ya juhudi za Serikali ya Rais Jakaya Kikwete ya kupunguza msongamano katika Jiji la Dar es salaam ambapo jana (leo) Tanzania imepata mkopo wa shilingi bilioni 52.5 kutoka Japan kwa ajili ya Ujenzi wa Barabara za Juu katika makutano ya TAZARA. Wengine ni Waziri wa Fedha Dkt . William Mgimwa(katikati) na Balozi wa Japan nchini Masaki Okada(kullia).Picha na GCU-HAZINA_Dodoma
---
Na Mwandishi Wetu GCU-HAZINA-Dodoma
Tanzania na Japan zimetiliana saini mkataba wa makubaliano wa mkopo wenye riba nafuu wa kuikopesha Tanzania shilingi bilioni 77.7 kwa ajili ya kutekeleza shughuli za  maendeleo hapa nchini.
Makabidhiano hayo yamefanyika leo(jana) mjini Dodoma ambapo kwa Tanzania iliwakilishwa na Waziri wa Fedha Dkt .William Mgimwa  na Balozi wa Japan nchini Masaki Okada.
Akizungumza mara baada ya kutiwa kwa saini makubaliano hayo Waziri wa Fedha Dkt. Mgimwa alisema kati ya fedha hizo shilingi bilioni 52.5 zitatumika katika ujenzi wa barabara ya juu kwa juu(daraja) katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam  .
Aliongeza kuwa kiasi kilichobaki ya shilingi bilioni 25.2 zitatumika katika kupunguza umaskini kwa fedha hizo kuingizwa katika Mfuko wa Bajeti( General Budget Supoort-GBS) .
Dkt. Mgimwa alisema kuwa mkopo huo umetolewa kwa masharti nafuu ambapo riba yake ni asilimia 0.01 na utalipwa kwa kipindi cha miaka 30 ambapo Tanzania itaanza kuulipa baada ya miaka 10 kutoka sasa.
Naye Balozi wa Japan nchini Masaki Okada alisema kuwa kukamilika kwa ujenzi wa daraja la juu katika makutano ya TAZARA utasaidia kupunguza msongamano katika Jiji la Dar es salaam na hivyo kupunguza muda wa watumiaji wa barabara za Jiji hilomkukaa katika foleni.
Alisema kuwa hatua hiyo itasaidia kuchochea ukuaji wa uchumi kwa kuwa wananchi wa Dar es salaam watakuwa na muda mrefu wa kufanya kazi kuliko kukaa katika foleni.
Naye Waziri wa Ujenzi Dkt. Jphn Magufuli alisema kuwa daraja hilo litakuwa na urefu wa Kilometa 1.2 na kuongeza kuwa kukamilika kwake itakuwa hatua mkombozi kwa wakazi wa Dar es salaam.
Alisema kuwa Serikali itaendelea kuboresha barabara mbalimbali za jiji la Dar es salaam ili kuhakikisha kuwa foleni katika mji huo zinapungua .
Aidha Dkt. Magufuli alitoa siku saba kwa wakazi walioko kandokando ya barabara ya Mwenge Morocco kubomoa nyumba zao zilizoko katika hifadhi ya barabara kabla Serikali hajaanza kutekeleza zoezi hilo kwa nguvu.
Alisema kuwa kimsingi wananchi wa eneo hilo walishalipwa fidia hivyo hawana sababu ya kuchelewesha upanuzi wa barabara hiyo ambapo inasababisha foleni kwa watumiaji.

NI ARNOLD KAYANDA NA ZAMARADI MKETEMA KUTOKA CLOUDS FM...!

Huyu jamaa wa kwanza kushoto mntabidi mnitajie jina lake!
 Katikati ni Arnold Kayanda halafu Zamaradi Mkitema kwa pampoja wana furahi kuniona King kif nawapiga picha ndani ya ukumbi wa  Double Tree , Masaki jijini Dar es Salaam .Pia unaweza kubonyeza...http://Wwwmasterkif.blogspot.com

KAULI YA SERIKALI KUHUSU KITITA CHA MILIONI 100 KWA MTU ATAKAYEMTAJA MTU ALIYERUSHA BOMU ARUSHA

Zifuatazo ni nukuu za maneno yaliyotolewa na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, sera, uratibu na bunge William Lukuvi kuhusu hilo bomu ambalo lililipuliwa kwenye mkutano cha Chadema Arusha.
“Mtu asiejulikana alirusha kitu katika kundi la watu kilichosababisha mlipuko mkubwa, mkutano huu ulikua na ulinzi wa jeshi la Polisi wakiwa na magari mawili… askari walisimama upande wa Kaskazini ya uwanja ambapo mrushaji alikua mashariki na alirusha bomu kuelekea Magharibi”
“Jaribio la Askari Polisi kutaka kumfata alierusha lilizuiwa na makundi ya Wananchi ambao walianza kuwashambulia polisi kwa mawe na kuwazomea na hivyo Polisi kulazimika kuanza kujiokoa badala ya kumsaka Muhalifu”
“Mlipuko huo ulisababisha watu wawili kufariki dunia ambao ni Judith William (48) na mtoto Ramadhan Juma (15) na watu 70 wamejeruhiwa miongoni mwao watatu wamejeruhiwa vibaya na wawili hali zao ni mbaya”
“Uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa mlipuko huo ulikuwa ni wa bomu la kurusha kwa mkono ambapo pia aina ya urushaji wa bomu hilo haitofautiani na mbinu iliyotumika kwenye shambulio jingine la bomu lililotokea kwenye kanisa la Olasiti Arusha”
“Kutokana na mfululizo wa matukio haya mageni, Serikali imeamua kutenga shilingi milioni 100 kama zawadi kwa mtu yeyote atakaeshirikiana na kutoa taarifa zitakazofanikisha kunaswa kwa muhalifu wa  matukio ya aina hii na mtandao wake mzima”

Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Mke wa hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere Waongoza Mamia ya Watanzania Kwenye Mazishi ya aliyekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,Marehemu Timoth Apiyo,yaliyofanyika nyumbani kwake kijiji cha Marasibora mkoani Mara.


 Waziri Mkuu, Mh. Mizengo Pinda akiweka udongo kaburini.
 Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Mzee Timoth Apiyo likiwazili Makaburini kwa kubebwa na Askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
 Jeneza likiingizwa kaburini.
Waziri Mkuu, Mh. Mizengo Pinda akiweka shada la maua kaburini.
Waziri Mkuu, Mh. Mizengo Pinda akijadiliana jambo na Mke wa hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere wakati wa msiba huo.
---
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda,ameongoza mamia ya waombolezaji kwenye mazishi ya aliyekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,Marehemu Timoth Apiyo,yaliyofanyika nyumbani kwake kijiji cha Marasibora mkoani Mara.

Waziri Pinda alitoa pole kwa familia na wakazi wa Kijiji cha Mara Sibora,Wilaya ya Rorya na Mkoa wa Mara kwa kumpoteza kiongozi na mzalendo aliyeitumikia nchi yake kwa uadilifu.

Wengine waliohudhuria maziko hayo ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu),William Lukuvi;Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue; Makatibu Mkuu Viongozi wastaafu, Balozi Paul Rupia, Balozi Marten Lumbanga na Philemon Luhanjo pamoja na mke wa hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere.

From The State House:President Jakaya Kikwete meets the Chairman and FIRST advisory council Rt. Hon Lord Hurd of Westwell


President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete meets with the Chairman and FIRST advisory council Rt. Hon Lord  Hurd of Westwell(right) in London this morning. Left is FIRST Chairman Mr. Rupert Goodman .FIRST is a multi-disciplinary International affairs organization founded in 1984 with the aim to enhance communication between leaders in industry, finance  and governance and to promote dialogue at the strategic level. President Kikwete is in London to attend the G8 open for Growth, Tax and Transparency event. Photo by Freddy Maro-State House

GERALD HANDO WA CLOUDS FM NUSURA AFUMULIWE NA BASTOLA YA KICHWA..!


MTANGAZAJI maarufu wa Clouds FM, Gerald Hando leo alfajiri alizua kizaazaa na kupelekea kutishiwa bastola na mtu ambaye jina lake halikufahamika mara moja.
Chanzo cha Saluti5 kimesema Hando aligonga gari la mtu huyo maeneo ya Kwa Kopa, jambo lililopelekea mtu huyo ashuke kwenye gari lake bastola ikiwa mkononi na kutishia kumfumua Hando.
Kama mtu huyo alidhani kutoa bastola ndio suluhisho basi alikosea sana, Gerald Hando anayetangaza kipindi cha "Power Breakfast" naye alishuka kwenye gari lake na kufungua shati lake na kuanza kumuamrisha mtu huyo afyatue bastola.
Huku akiporomosha matusi kwa ukali Hando alisema: “Piga hiyo bastola yako, shoot me.”
Hando aliendelea kuwa mkali huku akipigapiga kifua chake hali iliyovuta watu wengi kwenye tukio hilo ambao waliwasihi wote wawili kutuliza mzuka na kumfanya mtu huyo aliyekuwa na gari aina ya Rav 4 arudishe bastola yake kwenye gari na kutafuta njia nyingine ya kulimaliza tatizo lililotokea.Pia unaweza kubonyeza...http://www.masterkif.blogspot.com

BOMU ARUSHA... NJAMA NZITO


Na Joseph Ngilisho, Arusha
NYUMA ya matukio ya kigaidi ambayo yamefululiza kutokea jijini Arusha kuna njama nzito baada ya kuibuka maswali mengi yanayosababisha mahali hapa kutokuwa shwari na salama kufuatia bomu lililolipuliwa Jumamosi iliyopita, Uwazi lina uchambuzi.
Bomu hilo lililipuliwa katika mkutano wa Chadema wa kumaliza kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Kaloleni jijini hapa na kusababisha kuvunjika ghafla huku likiua watu wawili na wengine zaidi ya sitini kujeruhiwa.
Mlipuaji alilipua bomu hilo saa 11:50: jioni, dakika chache kabla ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe (pichani) kumaliza kuhutubia mkutano huo uliofanyika katika Viwanja vya Soweto jijini hapa na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi kisha kuacha maswali mengi.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo aliwataja waliofariki kuwa ni Judith William Mushi (46) ambaye alikuwa Katibu Kata wa Chadema, Kata ya Sokoni One na mkazi wa eneo hilo aliyemtaja kwa jina moja la Justine (16), mkazi wa Sombetini ambaye alifariki katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.
Tukio hilo ni la pili la bomu kulipuliwa katika mkusanyiko wa watu kwani Mei 5, mwaka huu bomu lililipuliwa katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti jijini hapa na kuua watu watatu na wengine kujeruhiwa.

JE, LILIMLENGA MBOWE?
Baadhi ya wanachama wa Chadema waliozungumza na Uwazi walidai kuwa bomu hilo la kurusha kwa mkono lililenga kumuua Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kutokana na sababu za kisiasa.
Wachunguzi walijiuliza kama mlipuaji alikuwa na nia ya  kumuua Mbowe na Lema kwa nini alitupa bomu kwa wananchi wakati viongozi hao walikuwa wanaonekana wakikusanya michango ya fedha kuchangia ununuzi wa maji kwa wasimamizi wao wa uchaguzi ulioahirishwa?
Pia swali lingine, kama hivyo ndivyo, kwa nini mlipuaji alirusha bomu wakati ambao Mbowe na Lema walikuwa wameshuka jukwaani?

CHADEMA WALIJIPIGA BOMU WENYEWE?
Wapo waliodai kuwa hujuma hizo ni mbinu za kisiasa zinazofanywa na wanasiasa wenye ufinyu wa mawazo huku wakijiuliza Chadema wanahusika?
Swali hilo lilijibiwa na baadhi ya wachambuzi wa kisiasa wakidai kuwa hawawezi kuhusika kutokana na ukweli kwamba hata kiongozi wao, Judith ameuawa na bomu hilo.

MRUSHA BOMU ALIOKOKAJE?
Watu mbalimbali wanajiuliza kama mrusha bomu alikuwa karibu na umati, aliwezaje kufanya unyama huo bila kukamatwa na wananchi waliomuona akirusha?
Pia katika mkutano huo kulikuwa na ulinzi wa polisi waliokuwa wakilinda usalama wa raia, ilikuwaje mrusha bomu huyo ambaye hakukamatwa, akaweza kuwatoroka hata wao (polisi)?

MLIPUAJI BOMU ANATAKA SERIKALI ICHUKIWE?
Wapo waliodai kuwa kama mrusha bomu yupo nje ya siasa, basi zinazofanyika ni njama nzito za kuwagombanisha wananchi na serikali yao ya awamu ya nne inayoongozwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, kitu ambacho serikali inapaswa kufanyia kazi.
“Kuna uwezekano labda ni haya makundi ya kigaidi na waasi kama M-23 na Al-Shaabab yanayolenga kuzivuruga serikali za Afrika Mashariki kwa kuzichonganisha na wananchi wake,” alisema Mzee Minja, kada wa Chadema mjini hapa.
Baadhi ya wananchi walisema mlipuaji alilenga kuua watu wengi na matokeo yake ni kwamba licha ya watu hao wawili kufariki dunia, majeruhi waliolazwa katika hospitali mbalimbali jijini hapa na KCMC mkoani Kilimanjaro, idadi iliyothibitishwa na polisi imefikia 60.
Habari zilieleza kuwa majeruhi wanne, hali zao zilikuwa mbaya huku mtoto, Farad Jamal (7), akiwa katika hali mbaya zaidi kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) katika Hospitali ya KCMC.
Mbowe amesema “ tukio hili ni kubwa na lina mambo mengi, chama kitawahudumia majeruhi wote.”
Kufuatia tukio hilo, msimamizi wa uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata nne, Jimbo la Arusha, Sipora Liana ambaye ni mkurugenzi wa jiji, alitangaza kuahirisha uchaguzi huo uliokuwa ufanyike juzi (Jumapili) hadi Juni 30, mwaka huu.
Liana alisema kuwa kuahirishwa kwa uchaguzi huo ni kutokana na hali tete iliyojitokeza Jumamosi na kusababisha uvunjifu wa amani hivyo kwa mtazamo huo usingeweza kufanyika kutokana na hali ya usalama kuwa mdogo.
Mkuu wa Mkoa, Mulongo alisema kuwa watu kadhaa wanashikiliwa na polisi wakihusishwa na tukio hilo na aliwasihi wananchi waendelee na shughuli zao wakati vyombo vya dola vikiendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

MAJERUHI WAZUNGUMZA
Akisimulia tukio hilo, mmoja wa majeruhi aliyelazwa katika Hospitali ya Seliani, Abdalah Alila (39) alisema kuwa akiwa katika mkutano huo majira ya saa 11.50 jioni, aliona kitu cheusi kikidondoka karibu yake na baadaye alisikia kishindo kizito.
“Ghafla nilijikuta chini na damu zikinichuruzika huku nikishindwa kutembea, nikatambaa kuomba msaada kwa watu waliokuwa wakikimbia hovyo,” alisema.

MRUSHA BOMU
Taarifa zilidai kuwa kuna mtu alionekana akirusha kitu kinachodaiwa kuwa ni bomu kwenye eneo la jukwaa karibu na gari la matangazo la chama hicho, lakini alipokuwa akifuatiliwa baada ya kutokea mlipuko huo, polisi nao walikuwa wameanza kudhibiti watu kwa kulipua mabomu ya kutoa machozi na kupiga risasi za moto, hali iliyozidisha vurugu.
Hali hiyo ilifanya barabara zote za Jiji la Arusha kujaa watu waliokuwa wakikimbia hovyo.
Kitendo cha watu kukimbia hovyo kuliwafanya polisi wengi kuingia mitaani kudhibiti watu na hivyo nao kulazimika kutumia mabomu ya machozi, hali ambayo ilizidisha taharuki.

BADO HOFU IMETANDA
Pamoja na viongozi kujitahidi kutuliza wananchi lakini bado hali ni tete jijini hapa kwa kuwa watu wana hofu hasa maeneo ambayo yana mkusanyiko wa watu wengi huku wengine wakijitahidi muda mwingi kuwa majumbani mwao.
Wananchi waliozungumza na Uwazi kwa nyakati tofauti kuhusu tukio hilo, wamemuomba Rais Kikwete kufuatilia kwa kina matukio hayo ili maswali yote yanayoulizwa hivi sasa yaweze kujibiwa japokuwa tayari amesema  serikali itafanya kila liwezekanalo kuwasaka waliohusika na kitendo hicho ili washitakiwe.Chanzo:www.globalpublishers.info

Isn't the G8 supposed to alleviate global tensions? Obama and Putin put on deeply awkward show of unity after disastrous meeting at summit


By LOUISE BOYLE
President Obama and Russian leader Vladimir Putin put on an almost comically awkward show of unity for the cameras today as they made virtually no eye contact and grimaced as the other spoke following a bilateral meeting at the G8 Summit.
Obama tilted his chair away from the Russian president who fidgeted with his fingers and tapped his feet.
Putin slumped down in his seat, leaned heavily on the arm rests and stared into the distance at the scenic backdrop of Lough Erne. The usually effusive Obama, who is never short of hugs for fellow leaders, did not raise a smile, his shoulders hunched and jaw working hard on a piece of gum.
Distant relations: President Obama looks grim as Russian president Vladimir Putin stares at the floor during a bilateral press conference at the Lough Erne resort near Enniskillen in Northern Ireland on Monday
Distant relations: President Obama looks grim as Russian president Vladimir Putin stares at the floor during a bilateral press conference at the Lough Erne resort near Enniskillen in Northern Ireland on Monday
Frosty: Obama glances away as he discusses the progress made at the meeting between the U.S. and Russia while Putin fidgeted with his hands
Frosty: Obama glances away as he discusses the progress made at the meeting between the U.S. and Russia while Putin fidgeted with his hands
Tough calls: Obama and Putin admitted that they did not agree over the their Syrian conflict as the U.S. arms rebel forces and Russian continues to back President Assad
Tough calls: Obama and Putin admitted that they did not agree over the their Syrian conflict as the U.S. arms rebel forces and Russian continues to back President Assad
The palpable tension in the room was evident after fraught discussions between the U.S. and Russia on Syria's bloody civil war.
Putin told Obama that their positions on Syria do not 'coincide' but they conceded that they have a shared interest in stopping the violence that has ravaged the Middle Eastern country during a two-year-old civil war.
Obama acknowledged in the bilateral meeting that they have a 'different perspective' on Syria but he said that both leaders wanted to address the fierce fighting and also wanted to secure chemical weapons in the country.
The words rang out hollowly in the press room as both leaders' body language appeared to show that little progress had been made on the brutal civil war which has left more than 90,000 Syrians dead.

Mtoto: Nilipigwa risasi na polisi


Arusha/Dodoma. Wakati watu waliofariki kwenye tukio la kurushwa bomu katika mkutano wa Chadema ikifikia watatu baada ya jana kufariki kwa mtoto Amir Ally (7), mtoto mwingine wa miaka kumi na moja aliyejeruhiwa, amedai kwamba alipigwa risasi na polisi kwenye tukio hilo
.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe naye ametoa tamko kuwa chama chake kina ushahidi wa kutosha wa watu waliohusika na tukio la kurushwa bomu katika mkutano wa kampeni wa chama hicho.
Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Arusha Medical Lutheran Center (ALMC), Dk Paul Kisanga alisema jana kuwa, Amir alifariki jana asubuhi baada ya kupata majeraha makubwa kichwani yaliyodhuru ubongo wake.
Dk Kisanga alisema huyo ni mmoja wa watoto watano, waliojeruhiwa wakati wakitoka madrasa huko Kaloleni, jirani na Uwanja wa Soweto kulipokuwa na mkutano na alifariki jana asubuhi hospitalini hapo.
Alisema watoto wengine wawili ambao ni ndugu; Fatuma na Sharifa Jumanne wamepelekwa Nairobi kwa matibabu zaidi baada ya miili yao kukutwa na vyuma.

Dk Kisanga aliwataja watoto wengine waliojeruhiwa kuwa ni Fahad Jamal (7) ambaye yupo ICU akisubiri timu ya madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na hali yake kutoruhusu kusafirishwa. Pia yupo Abubakar Adam (11) ambaye amejeruhiwa mguuni na amelazwa katika Hospitali ya Mkoa, Mount Meru.
Mtoto aeleza kupigwa risasi
Adam alisema jana kuwa alipigwa risasi na mtu aliyekuwa amevalia sare za polisi, wakati akitoka madrasa akiwa na ndugu yake, Fahdi katika eneo la Soweto.
Alisema akiwa njiani, aliona watu wakimkimbiza mtu na ghafla alishangaa kupigwa risasi na kuanguka chini.
“Namkumbuka aliyenipiga risasi alikuwa amevaa sare za polisi,” alisema Adam mwanafunzi katika Shule ya Msingi Levolosi huku akitokwa machozi.

Monday, June 17, 2013

'I'm looking for an Abraham Lincoln without the beard': Judge reveals unusual criteria for Miss USA contestants as Connecticut 25-year-old wins Donald Trump's coveted crown


By DAILY MAIL REPORTER
One of the judges of this year's Miss USA competition declared on Sunday night that he was looking for a winner who reminded him of Abraham Lincoln 'without the beard' before 25-year-old Connecticut beauty Erin Brady was crowned in Donald Trump's coveted contest.
'Wait Wait ... Don't Tell Me' personality Mo Rocca offered up his bizarre criteria as the contestants strutted their stuff in elegant gowns and swimsuits.
Shortly after, Brady, of South Glastonbury, was announced the winner of the beauty pageant, which took place at the Planet Hollywood hotel-casino in Las Vegas.
 Erin Brady
Hooray: Miss Connecticut Erin Brady reacts as she is crowned by Miss USA 2012 Nana Meriwether during the Miss USA pageant at the Planet Hollywood Resort and Casino in Las Vegas, Nevada
Winner: Miss Connecticut Erin Brady, center, beat 50 other hopefuls to win
Winner: Miss Connecticut Erin Brady, center, beat 50 other hopefuls to win
Emotional: Miss Connecticut USA 2013 Erin Brady was overcome when she was announced as Miss USA 2013
Emotional: Miss Connecticut USA 2013 Erin Brady was overcome when she was announced as Miss USA 2013 on Sunday night

HEBU CHEKI JINSI LANGA ALIVYOZIKWA MAKABURI YA KINONDONI JIJINI DAR


Jeneza lenye mwili wa Langa likiwe mbele ya waombolezaji.
Dk. Cheni akiuaga mwili wa Langa.
Ridhiwan Kikwete akitoa heshima zake za mwisho kwa marehemu..
Prodyuza P Funky akiaga.
Mtangazaji Adam Mchomvu akitoa heshima zake.
Kala Jeremiah akimuaga Mwana Hip Hop mwenzake.
Jokate Mwegelo naye akitoa heshima zake za mwisho.
DJ Choka akiaga.
Miraji Kikwete akiuaga mwili wa Langa.
C Pwaa akitoa heshima za mwisho.
Dada wa marehemu Langa akilia kwa uchungu.
Mwili wa marehemu ukipelekwa kwenye gari tayari kwa safari ya makaburini.
Jeneza la likiwa kwenye gari kuelekea makaburini.Chanzo:www.globalpublishers.info