Ni Lulu Semagongo aka lulu Kimwana akiwa ndani ya ukumbi wa Mango Garden maeneo ya Kinondoni huku African Stars wakitoa burudani kwa kwenda mbele! Pia unaweza kubonyeza...http://Wwwmasterkif.blogspot.com
Wednesday, June 19, 2013
DIAMOND : PREZZO KWANGU HANA LOLOTE
Kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu:Waziri Mkuu Mizengo Pinda Amjulia Hali Wabunge wa Chadema Mbunge wa Arumeru Mashariki-Chadema , Joshua Nasari ambaye amelazwa katika hospitali ya Serian Arusha anakotibiwa kwa madai ya kushambuliwa na wananchi eneo la Makuyuni na Mbunge wa Viti Maalum, Namelok Sokoinine aliyelazwa kwenye hospitali ya Serian Arusha baada ya kuvunjika mguu akiwa nyumbani kwake.
Waziri
mkuu, Mizengo Pinda akimpa pole mbunge wa Arumeru Mashariki-Chadema , Joshua
Nasari ambaye amelazwa katika hospitali ya Serian Arusha anakotibiwa
kwa madai ya kushambuliwa na wananchi eneo la Makuyuni. 
Waziri
mkuu, Mizengo Pinda akimpa pole Mbunge wa Viti Maalum, Namelok
Sokoinine aliyelazwa kwenye hospitali ya Serian Arusha baada ya
kuvunjika mguu akiwa nyumbani kwake.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
OMMY DIMPOZ AOMBA MSAMAHA
Na Mwandishi WetuKUFUATIA kumtusi marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ kuwa amekufa maskini, mmiliki wa akaunti inayodaiwa ni ya msanii Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ katika mtandao wa Facebook, amewaomba msamaha Watanzania kwa kitendo chake hicho baada ya kumwagiwa mitusi.
Katika akaunti hiyo yenye jina la Ommy Dimpoz- Omary Faraji, mwishoni mwa wiki iliyopita ilijaa matusi na maneno makali yakimnanga jamaa huyo kwa kauli yake aliyoitoa hivi karibuni kwenye Tuzo za…
Na Mwandishi WetuKUFUATIA kumtusi marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ kuwa amekufa maskini, mmiliki wa akaunti inayodaiwa ni ya msanii Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ katika mtandao wa Facebook, amewaomba msamaha Watanzania kwa kitendo chake hicho baada ya kumwagiwa mitusi.
Katika akaunti hiyo yenye jina la Ommy Dimpoz- Omary Faraji, mwishoni mwa wiki iliyopita ilijaa matusi na maneno makali yakimnanga jamaa huyo kwa kauli yake aliyoitoa hivi karibuni kwenye Tuzo za Kili.
Aliandika: “Binadamu ni kukosea mara nyingi na-regret (kujuta) kwa yale niliyosema kuhusu Ngwea. Kama ningekuwa na uwezo wa kurudisha siku na maneno nyuma, yale ndo yangekuwa ya kwanza.
“Nakubali nilifanya kosa kubwa sana na nikaweka pride (majivuno) yangu na sifa zangu mbele bila kufikiria nitakayosema.
“Nyumbani Tanzania, Bongo nimeenda hadi kwa redio stations kuwaomba msamaha.
“Team Kigoma All Stars na wasanii wenzangu wa Bongo, Kenya, Uganda na nchi nyingine zote nisameheni tafadhali.
“I have learnt to think about what I say before I Talk or let it out of my mouth (Nimejifunza kufikiri chakusema kabla ya kukizungumza au kukiacha kitoke mdomoni mwangu).
“Nimewakosea familia ya Ngwea na ma-fans (mashabiki) wangu wanaonipenda hata pia kwa Allah Mungu Baba, naombeni msamaha tafadhali.”
Pamoja na kuomba msamaha bado watu waliendelea kumponda wakihoji ni kitu gani Ngwea alimfanyia huku mwanamuziki Khaleed Mohamed ‘TID Mnyama’ akiahidi kumpa kichapo.Baada ya kuomba msamaha, msanii huyo anayechipukia alidaiwa kupanga safari ya kwenda Morogoro kuiomba msamaha familia ya Ngwea.Chanzo:www.globalpublishers.info
YAYA TOURE ANALIPWA MILIONI 400 KWA WIKI(FEDHA YA KITANZANIA)
Unaweza kusema kuwa leo King kif nafanya utani!Jamani ni kweli mchezaji huyu analipwa kiasi hicho cha pesa.wiki iliyopita wakati Taifa stars ilipocheza na Ivory Coast , mchezaji huyu alikuwa makini na hakuwa na pupa kabisa uwanjani.Mara nyingi ukimuona mchezaji anafanya hivyo , bas tambua kuwa anauwezo mkubwa wa kucheza mpira.
Pia unaweza kubonyeza...http://Wwwmasterkif.blogspot.com
Arfi, Lissu watiwa mbaroni Arusha
Arusha. Wabunge wanne wa Chadema, Said Arfi (Mpanda Mjini), Tundu Lissu
(Singida Mashariki), Mustapha Akunaay (Mbulu) na Joyce Mukya (Viti
Maalumu) wamekamatwa wakituhumiwa kuhusika na mkusanyiko usio halali
kwenye Uwanja wa Soweto jana.

Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja alisema jana kwamba
pamoja na wabunge hao pia wamewakamata watu wapatao 60 kutokana na
vurugu zilizozuka jana baada ya Polisi kuwatawanya kwenye uwanja huo
waliokuwa wamekusanyika kuomboleza vifo vya watu watatu;
Judith Moshi, Ramadhan Juma na Amir Ally waliofariki kwenye mlipuko wa bomu uliotokea kwenye uwanja huohuo, Jumamosi iliyopita.
Mbali ya viongozi hao, alisema wanawasaka Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.
“Tunawasaka wabunge ili tuwajumuishe na watu hawa kwa kosa la kuhusika
na mkusanyiko usiokuwa halali. Hadi sasa tumefanikiwa kulinasa gari la
Mbowe,” alisema Chagonja.
Pia kamatakamata hiyo imemkumba Mpigapicha wa Kituo cha Televisheni cha
Channel Ten, Ashraf Bakari. Polisi walilazimika kutumia nguvu
kuwatawanya waombolezaji hao.
Awali, Kamishna Chagonja alisema jana asubuhi kuwa wamelazimika kuzuia
viwanja hivyo kutumika baada ya wamiliki wake, AICC kuzuia shughuli za
Chadema kwenye eneo lao.
Kamishna Chagonja aliwaonyesha waandishi wa habari barua aliyosema
imeandikwa na uongozi wa AICC kuzua Chadema kuendelea kuutumia Uwanja wa
Soweto.
Mabomu yarindima
Dalili za kuzuka kwa vurugu zilianza kuonekana asubuhi baada ya polisi
kuzingira uwanja huo na kuzuia watu waliokuwa wameanza kufurika katika
eneo hilo kuanzia saa moja kuingia kwa ajili ya maombolezo.
GERALD HANDO NUSURA AUAWE
Na Sifae PaulMTANGAZAJI mwenye jina kubwa wa Radio Clouds FM, Gerald Hando ‘Mzee Mnoko’ ameponea chupuchupu kuuawa baada ya kutishiwa kwa bastola.
Kwa mujibu wa chanzo makini, tukio hilo lilijiri maeneo ya Mwananyamala Kwa Kopa, Dar alfajiri ya Jumatatu wiki hii.
Ilikuwaje?
Baada ya kutonywa mkasa huo, gazeti hili liliwasiliana na Hando ambaye siku hiyo alishindwa kutokea kwenye kipindi chake cha Power Breakfast na alielezea kisa kizima.
Alisema: “Ilikuwa saa 12:40 wakati nakatiza pale Kwa Kopa, kabla sijaingia barabara ya kuelekea Ali Hassan Mwinyi, ghafla lilitokea gari aina ya RAV4. Lilikuwa limebana sana upande wangu, ghafla nikasikia kama limenigonga, niliposhusha kioo, kweli nikaona gari langu limegongwa.
“Nilichungulia kwenye lile gari nikamuuliza dereva kwa ishara vipi?
“Nilipoona hanijibu nilifunga vioo vya gari langu nikawa nimetulia, nikapigwa na butwaa kumuona yule jamaa ameshuka akiwa na bastola.
“Alinigongea kioo lakini sikufungua, nilikuwa nimetaharuki sielewi nini kinaendelea. Lakini wakati ananitishia kuwa nishuke anipige, kuna mwanamke alikuwa naye kwenye gari lake ambaye alishuka na kumlazimisha warudi kwenye gari lao.
“Akiwa ndani ya gari lake, jamaa alifyatua risasi iliyovunja kioo cha mbele cha gari lake na sijui risasi ilielekea wapi maana nilikuwa nimeshachanganyikiwa.
“Kama hiyo haitoshi, jamaa alishuka kwa mara nyingine akiwa na hasira sana na kunifuata tena akitaka kunifyatulia risasi, alipoona imeshindikana alipasua tairi za kushoto za gari langu huku akiniambia ndiyo mchezo umeanza nitaona.
“Bahati nzuri polisi walishafika eneo la tukio kwa sababu ishu yenyewe ilichukua muda mrefu, tulichukuliwa wote hadi Oysterbay (kituo cha polisi) nikatoa maelezo yangu na kumfungulia jalada la kesi namba OB/RB/10613/13 (SHAMBULIO),” alisimulia Hando.
Hadi tunakwenda mitamboni sakata hilo halikujulikana hatma yake, tunaahidi kuendelea kulifuatilia.
Chanzo:www.globalpublishers.info
Tanzania set to reap from Obama’s visit
By CHABY BARASA
Tanzania has said it will capitalise on the forthcoming visit by United
States President Barack Obama to promote bilateral ties between the two
countries.

President Jakaya Kikwete
President Jakaya Kikwete said the US has been one of his country’s
important development partners and noted that the visit ‘’would further
cement the existing good ties.’’
“The US is our long time ally. We have important programmes in areas
like infrastructure and health under the MCC and PEPFAR which have been a
huge success so far,” said Mr Kikwete when fielding questions from the
media here on Sunday.
Under the Millennium Challenge Corporation, Tanzania and USA signed a
compact agreement for the 698 million US dollar-grant, for a period of
five year in 2008. The money was meant to help fund infrastructure
projects in line with Tanzania’s poverty alleviation initiatives.
Through the US President’s Emergency Plan for AIDS Relief, Tanzania has
received 1076.4 million US dollars to support comprehensive HIV/AIDS
prevention, treatment and care programmes from 2009 to 2011.
International Sickle Cell Day Campaign
19th
June marks World Sickle Cell Day. Please support the initiative by
posting or making this your profile picture on your Facebook page.
Pia unaweza kuingia ...http://Wwwmasterkif.blogspot.com
Tuesday, June 18, 2013
VODACOM YAPANUA WIGO HUDUMA NA AJIRA KWA WATANZANIA
---
• Watanzania zaidi kuendelea kupata huduma za mawasilianoDar Es Salaam, June 18, 2013 … Huku jiji la Dar es Salaam likiendelea kukua kwa kasi na kushuhudia ongezeko kubwa la watu kutoka sehemu mbalimbali, upatikanaji wa huduma mbalimbali za kijamii umekuwa ukikabiliwa na changamoto kadhaa kutokana na kasi ya utoaji huduma kutoendana na kasi ya ongezeko la watu.
Katika kukidhi haja hiyo ya utoaji wa huduma kwa wateja na elimu kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam, Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania imeendelea kupanua wigo wa ajira na huduma kwa kufungua duka la huduma kwa wateja katika jengo la Milenium Tower lililoko Makumbusho jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia wakati wa uzinduzi wa duka hilo, Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Joseline Kamuhanda, amesema Vodacom ni kampuni pekee ambayo imeendelea kuongoza kwa kuwa na maduka mengi ya mauzo na huduma kwa wateja kwa kufikisha maduka 66 ikiwa ni kampuni pekee kuwa na maduka mengi ya huduma na kufanikisha adhma ya kukidhi mahitaji ya huduma kwa wateja wa kampuni hiyo, huku Dar es Salaam ikiwa na idadi ya maduka 21.
“Ukuaji wa huduma kwa kampuni ya Vodacom umekuwa kwa kasi, huduma kama ya M – Pesa sasa imepanuka kwa kasi na kutoa huduma kwa watanzania zaidi ya milioni 10. Kufuatia mafaanikio haya tunalazimika kuhakikisha upatikanaji wa huduma kwa wateja ni wa uhakika” alisema Kamuhanda na kuongeza kuwa,
“Kuongoza katika sekta ya mawasilaino kuna changamoto zake, lazima tuhakikishe tunaendana na kasi ya ukuaji na ongezeko la watu na uhitaji wa huduma zetu kwa watu wa aina mbalimbali.
Aidha Kamuhanda alisema kuwa Kufunguliwa kwa duka hilo sasa sio tu kunaboresha upatikanaji wa huduma pia ni fursa pekee ya kuendelea kupanua wigo wa ajira kwa watanzania.
“Ufunguzi wa duka hili unatoa fursa ya ajira kwa watanzania, ambapo wafanyakazi wapatao 3 watatoa huduma kwa wateja wetu hivyo ni hatua kubwa kwa kutengeneza ajira kwa wafanyakazi wapya. Hadi kufikia sasa, Vodacom imetoa ajira za moja kwa moja kwa wafanyakazi 500 na wengine zaidi ya 450,000 wenye ajira zisizo rasmi,” alisema Kamuhanda.
Tanzania na Japan zimetiliana saini mkataba wa makubaliano wa mkopo wenye riba nafuu wa kuikopesha Tanzania shilingi bilioni 77.7 kwa ajili ya kutekeleza shughuli za maendeleo hapa nchini Pamoja na ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini

Waziri
wa Fedha Dkt .William Mgimwa (katikati ) na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Japan hapa nchini(JICA) Yasunori Onishi(kulia)wakisaini
hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu ambapo Japan itaikopesha
Tanzania shilingi bilioni 77.7 kwa ajili ujenzi wa barabara ya juu kwa
juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam na fedha nyingine
zitasaidia katika kupunguza umaskini. Sherehe zilifanyika jana (leo)
mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Waziri wa Ujenzi Dkt. John
Magufuli(kushoto)

Waziri
wa Fedha Dkt .William Mgimwa (katikati ) na Balozi wa Japan nchini
Masaki Okada(kulia)wakisaini hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu
ambapo Japan itaikopesha Tanzania shilingi bilioni 77.7 kwa ajili
ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar
es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini.
Sherehe zilifanyika jana (leo) mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Waziri wa
Ujenzi Dkt. John Magufuli(kushoto)

Mwakilishi
wa Shirika la Maendeleo la Japan hapa nchini(JICA) Yasunori
Onishi(kulia) na Waziri wa Fedha wakibadilishana hati ya ujenzi wa
daraja la juu katika makutano ya TAZARAjana(leo) mjini Dodoma wakati wa
sherehe za kusaini hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu ambapo
Japan itaikopesha Tanzania shilingi bilioni 77.7 kwa ajili ujenzi wa
barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam
na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini. Wengine ni
Balozi wa Japan nchini Masaki Okada ( kulia) , na Waziri wa Ujenzi
Dkt. John Magufuli(katikati)

Waziri
wa Fedha Dkt .William Mgimwa (kushoto) na Balozi wa Japan nchini Masaki
Okada(kulia)wakibadilishana hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu
ambapo Japan itaikopesha Tanzania shilingi bilioni 77.7 kwa ajili
ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar
es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini.
Sherehe zilifanyika jana (leo) mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Waziri wa
Ujenzi Dkt. John Magufuli(katikati)

Mwakilishi
wa Shirika la Maendeleo la Japan hapa nchini(JICA) Yasunori
Onishi(kulia) akielezea mkakati watakaoutumia katika ujenzi wa daraja
la juu katika makutano ya TAZARAjana(leo) mjini Dodoma wakati wa sherehe
za kusaini hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu ambapo Japan
itaikopesha Tanzania shilingi bilioni 77.7 kwa ajili ujenzi wa
barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam
na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini. Wengine ni
Balozi wa Japan nchini Masaki Okada ( wa pili kutoka kulia) , Waziri wa
Fedha Dkt William Mgimwa (wa pili kushoto) na Waziri wa Ujenzi Dkt.
John Magufuli(kushoto)

Balozi
wa Japan nchini Masaki Okada(kulia) akizungumza na waandishi wa habari
jana (leo) mjini Dodoma mara baada yake kusaini na Tanzania hati ya
makubaliano ya mkopo wa riba nafuu ambapo Japan itaikopesha Tanzania
shilingi bilioni 77.7 kwa ajili ujenzi wa barabara ya juu kwa juu
katika makutano ya TAZARA jijini Dar es salaam na fedha nyingine
zitasaidia katika kupunguza umaskini. Wengine ni Waziri wa Fedha Dkt
.William Mgimwa (katikati) na Waziri wa Ujenzi Dkt. John
Magufuli(kushoto)

Waziri
wa Fedha Dkt .William Mgimwa (kushoto) na Balozi wa Japan nchini Masaki
Okada(kulia)wakibadilishana hati ya makubaliano ya mkopo wa riba nafuu
ambapo Japan itaikopesha Tanzania shilingi bilioni 77.7 kwa ajili
ujenzi wa barabara ya juu kwa juu katika makutano ya TAZARA jijini Dar
es salaam na fedha nyingine zitasaidia katika kupunguza umaskini.
Sherehe zilifanyika jana (leo) mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Waziri wa
Ujenzi Dkt. John Magufuli(katikati)

Dr. Magufuli—Waziri wa Ujenzi Dkt.
John Magufuli(kushoto) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari
jana(leo) mjini Dodoma juuu ya juhudi za Serikali ya Rais Jakaya
Kikwete ya kupunguza msongamano katika Jiji la Dar es salaam ambapo jana
(leo) Tanzania imepata mkopo wa shilingi bilioni 52.5 kutoka Japan kwa
ajili ya Ujenzi wa Barabara za Juu katika makutano ya TAZARA. Wengine ni
Waziri wa Fedha Dkt . William Mgimwa(katikati) na Balozi wa Japan
nchini Masaki Okada(kullia).Picha na GCU-HAZINA_Dodoma
---
Na Mwandishi Wetu GCU-HAZINA-Dodoma
Tanzania
na Japan zimetiliana saini mkataba wa makubaliano wa mkopo wenye riba
nafuu wa kuikopesha Tanzania shilingi bilioni 77.7 kwa ajili ya
kutekeleza shughuli za maendeleo hapa nchini.
Makabidhiano
hayo yamefanyika leo(jana) mjini Dodoma ambapo kwa Tanzania
iliwakilishwa na Waziri wa Fedha Dkt .William Mgimwa na Balozi wa Japan
nchini Masaki Okada.
Akizungumza
mara baada ya kutiwa kwa saini makubaliano hayo Waziri wa Fedha Dkt.
Mgimwa alisema kati ya fedha hizo shilingi bilioni 52.5 zitatumika
katika ujenzi wa barabara ya juu kwa juu(daraja) katika makutano ya
TAZARA jijini Dar es salaam .
Aliongeza
kuwa kiasi kilichobaki ya shilingi bilioni 25.2 zitatumika katika
kupunguza umaskini kwa fedha hizo kuingizwa katika Mfuko wa Bajeti(
General Budget Supoort-GBS) .
Dkt.
Mgimwa alisema kuwa mkopo huo umetolewa kwa masharti nafuu ambapo riba
yake ni asilimia 0.01 na utalipwa kwa kipindi cha miaka 30 ambapo
Tanzania itaanza kuulipa baada ya miaka 10 kutoka sasa.
Naye
Balozi wa Japan nchini Masaki Okada alisema kuwa kukamilika kwa ujenzi
wa daraja la juu katika makutano ya TAZARA utasaidia kupunguza
msongamano katika Jiji la Dar es salaam na hivyo kupunguza muda wa
watumiaji wa barabara za Jiji hilomkukaa katika foleni.
Alisema
kuwa hatua hiyo itasaidia kuchochea ukuaji wa uchumi kwa kuwa wananchi
wa Dar es salaam watakuwa na muda mrefu wa kufanya kazi kuliko kukaa
katika foleni.
Naye
Waziri wa Ujenzi Dkt. Jphn Magufuli alisema kuwa daraja hilo litakuwa
na urefu wa Kilometa 1.2 na kuongeza kuwa kukamilika kwake itakuwa hatua
mkombozi kwa wakazi wa Dar es salaam.
Alisema
kuwa Serikali itaendelea kuboresha barabara mbalimbali za jiji la Dar
es salaam ili kuhakikisha kuwa foleni katika mji huo zinapungua .
Aidha
Dkt. Magufuli alitoa siku saba kwa wakazi walioko kandokando ya
barabara ya Mwenge Morocco kubomoa nyumba zao zilizoko katika hifadhi ya
barabara kabla Serikali hajaanza kutekeleza zoezi hilo kwa nguvu.
Alisema
kuwa kimsingi wananchi wa eneo hilo walishalipwa fidia hivyo hawana
sababu ya kuchelewesha upanuzi wa barabara hiyo ambapo inasababisha
foleni kwa watumiaji.
NI ARNOLD KAYANDA NA ZAMARADI MKETEMA KUTOKA CLOUDS FM...!
Huyu jamaa wa kwanza kushoto mntabidi mnitajie jina lake!
Katikati ni Arnold Kayanda halafu Zamaradi Mkitema kwa pampoja wana furahi kuniona King kif nawapiga picha ndani ya ukumbi wa Double Tree , Masaki jijini Dar es Salaam .Pia unaweza kubonyeza...http://Wwwmasterkif.blogspot.com
Katikati ni Arnold Kayanda halafu Zamaradi Mkitema kwa pampoja wana furahi kuniona King kif nawapiga picha ndani ya ukumbi wa Double Tree , Masaki jijini Dar es Salaam .Pia unaweza kubonyeza...http://Wwwmasterkif.blogspot.com
KAULI YA SERIKALI KUHUSU KITITA CHA MILIONI 100 KWA MTU ATAKAYEMTAJA MTU ALIYERUSHA BOMU ARUSHA
Zifuatazo ni nukuu za maneno yaliyotolewa na Waziri wa nchi
Ofisi ya Rais, sera, uratibu na bunge William Lukuvi kuhusu hilo bomu
ambalo lililipuliwa kwenye mkutano cha Chadema Arusha.
“Mtu asiejulikana alirusha kitu katika kundi la watu
kilichosababisha mlipuko mkubwa, mkutano huu ulikua na ulinzi wa jeshi
la Polisi wakiwa na magari mawili… askari walisimama upande wa Kaskazini
ya uwanja ambapo mrushaji alikua mashariki na alirusha bomu kuelekea
Magharibi”
“Jaribio la Askari Polisi kutaka kumfata alierusha lilizuiwa
na makundi ya Wananchi ambao walianza kuwashambulia polisi kwa mawe na
kuwazomea na hivyo Polisi kulazimika kuanza kujiokoa badala ya kumsaka
Muhalifu”
“Mlipuko huo ulisababisha watu wawili kufariki dunia ambao ni
Judith William (48) na mtoto Ramadhan Juma (15) na watu 70 wamejeruhiwa
miongoni mwao watatu wamejeruhiwa vibaya na wawili hali zao ni mbaya”
“Uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa mlipuko huo ulikuwa ni wa
bomu la kurusha kwa mkono ambapo pia aina ya urushaji wa bomu hilo
haitofautiani na mbinu iliyotumika kwenye shambulio jingine la bomu
lililotokea kwenye kanisa la Olasiti Arusha”
“Kutokana na mfululizo wa matukio haya mageni, Serikali
imeamua kutenga shilingi milioni 100 kama zawadi kwa mtu yeyote
atakaeshirikiana na kutoa taarifa zitakazofanikisha kunaswa kwa muhalifu
wa matukio ya aina hii na mtandao wake mzima”
Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Mke wa hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere Waongoza Mamia ya Watanzania Kwenye Mazishi ya aliyekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,Marehemu Timoth Apiyo,yaliyofanyika nyumbani kwake kijiji cha Marasibora mkoani Mara.
Waziri Mkuu, Mh. Mizengo Pinda akiweka udongo kaburini.
Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Mzee Timoth Apiyo likiwazili Makaburini kwa kubebwa na Askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
Jeneza likiingizwa kaburini.
Waziri Mkuu, Mh. Mizengo Pinda akiweka shada la maua kaburini.
Waziri Mkuu, Mh. Mizengo Pinda akijadiliana jambo na Mke wa hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere wakati wa msiba huo.
---
WAZIRI
Mkuu Mizengo Pinda,ameongoza mamia ya waombolezaji kwenye mazishi ya
aliyekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,Marehemu Timoth Apiyo,yaliyofanyika
nyumbani kwake kijiji cha Marasibora mkoani Mara.
Waziri
Pinda alitoa pole kwa familia na wakazi wa Kijiji cha Mara
Sibora,Wilaya ya Rorya na Mkoa wa Mara kwa kumpoteza kiongozi na
mzalendo aliyeitumikia nchi yake kwa uadilifu.
Wengine
waliohudhuria maziko hayo ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano
na Uratibu),William Lukuvi;Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue;
Makatibu Mkuu Viongozi wastaafu, Balozi Paul Rupia, Balozi Marten
Lumbanga na Philemon Luhanjo pamoja na mke wa hayati Baba wa Taifa, Mama
Maria Nyerere.
From The State House:President Jakaya Kikwete meets the Chairman and FIRST advisory council Rt. Hon Lord Hurd of Westwell
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete meets with the Chairman and FIRST advisory council Rt. Hon Lord Hurd
of Westwell(right) in London this morning. Left is FIRST Chairman Mr.
Rupert Goodman .FIRST is a multi-disciplinary International affairs
organization founded in 1984 with the aim to enhance communication
between leaders in industry, finance and
governance and to promote dialogue at the strategic level. President
Kikwete is in London to attend the G8 open for Growth, Tax and
Transparency event. Photo by Freddy Maro-State House
GERALD HANDO WA CLOUDS FM NUSURA AFUMULIWE NA BASTOLA YA KICHWA..!
MTANGAZAJI maarufu wa Clouds FM, Gerald Hando leo alfajiri alizua kizaazaa na kupelekea kutishiwa bastola na mtu ambaye jina lake halikufahamika mara moja.
Chanzo cha Saluti5 kimesema Hando aligonga gari la mtu huyo maeneo ya Kwa Kopa, jambo lililopelekea mtu huyo ashuke kwenye gari lake bastola ikiwa mkononi na kutishia kumfumua Hando.
Kama mtu huyo alidhani kutoa bastola ndio suluhisho basi alikosea sana, Gerald Hando anayetangaza kipindi cha "Power Breakfast" naye alishuka kwenye gari lake na kufungua shati lake na kuanza kumuamrisha mtu huyo afyatue bastola.
Huku akiporomosha matusi kwa ukali Hando alisema: “Piga hiyo bastola yako, shoot me.”
Hando aliendelea kuwa mkali huku akipigapiga kifua chake hali iliyovuta watu wengi kwenye tukio hilo ambao waliwasihi wote wawili kutuliza mzuka na kumfanya mtu huyo aliyekuwa na gari aina ya Rav 4 arudishe bastola yake kwenye gari na kutafuta njia nyingine ya kulimaliza tatizo lililotokea.Pia unaweza kubonyeza...http://www.masterkif.blogspot.com
BOMU ARUSHA... NJAMA NZITO
Na Joseph Ngilisho, ArushaNYUMA ya matukio ya kigaidi ambayo yamefululiza kutokea jijini Arusha kuna njama nzito baada ya kuibuka maswali mengi yanayosababisha mahali hapa kutokuwa shwari na salama kufuatia bomu lililolipuliwa Jumamosi iliyopita, Uwazi lina uchambuzi.
Bomu hilo lililipuliwa katika mkutano wa Chadema wa kumaliza kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Kaloleni jijini hapa na kusababisha kuvunjika ghafla huku likiua watu wawili na wengine zaidi ya sitini kujeruhiwa.
Mlipuaji alilipua bomu hilo saa 11:50: jioni, dakika chache kabla ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe (pichani) kumaliza kuhutubia mkutano huo uliofanyika katika Viwanja vya Soweto jijini hapa na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi kisha kuacha maswali mengi.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo aliwataja waliofariki kuwa ni Judith William Mushi (46) ambaye alikuwa Katibu Kata wa Chadema, Kata ya Sokoni One na mkazi wa eneo hilo aliyemtaja kwa jina moja la Justine (16), mkazi wa Sombetini ambaye alifariki katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.
Tukio hilo ni la pili la bomu kulipuliwa katika mkusanyiko wa watu kwani Mei 5, mwaka huu bomu lililipuliwa katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti jijini hapa na kuua watu watatu na wengine kujeruhiwa.
JE, LILIMLENGA MBOWE?
Baadhi ya wanachama wa Chadema waliozungumza na Uwazi walidai kuwa bomu hilo la kurusha kwa mkono lililenga kumuua Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kutokana na sababu za kisiasa.
Wachunguzi walijiuliza kama mlipuaji alikuwa na nia ya kumuua Mbowe na Lema kwa nini alitupa bomu kwa wananchi wakati viongozi hao walikuwa wanaonekana wakikusanya michango ya fedha kuchangia ununuzi wa maji kwa wasimamizi wao wa uchaguzi ulioahirishwa?
Pia swali lingine, kama hivyo ndivyo, kwa nini mlipuaji alirusha bomu wakati ambao Mbowe na Lema walikuwa wameshuka jukwaani?
CHADEMA WALIJIPIGA BOMU WENYEWE?
Wapo waliodai kuwa hujuma hizo ni mbinu za kisiasa zinazofanywa na wanasiasa wenye ufinyu wa mawazo huku wakijiuliza Chadema wanahusika?
Swali hilo lilijibiwa na baadhi ya wachambuzi wa kisiasa wakidai kuwa hawawezi kuhusika kutokana na ukweli kwamba hata kiongozi wao, Judith ameuawa na bomu hilo.
MRUSHA BOMU ALIOKOKAJE?
Watu mbalimbali wanajiuliza kama mrusha bomu alikuwa karibu na umati, aliwezaje kufanya unyama huo bila kukamatwa na wananchi waliomuona akirusha?
Pia katika mkutano huo kulikuwa na ulinzi wa polisi waliokuwa wakilinda usalama wa raia, ilikuwaje mrusha bomu huyo ambaye hakukamatwa, akaweza kuwatoroka hata wao (polisi)?
MLIPUAJI BOMU ANATAKA SERIKALI ICHUKIWE?
Wapo waliodai kuwa kama mrusha bomu yupo nje ya siasa, basi zinazofanyika ni njama nzito za kuwagombanisha wananchi na serikali yao ya awamu ya nne inayoongozwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, kitu ambacho serikali inapaswa kufanyia kazi.
“Kuna uwezekano labda ni haya makundi ya kigaidi na waasi kama M-23 na Al-Shaabab yanayolenga kuzivuruga serikali za Afrika Mashariki kwa kuzichonganisha na wananchi wake,” alisema Mzee Minja, kada wa Chadema mjini hapa.
Baadhi ya wananchi walisema mlipuaji alilenga kuua watu wengi na matokeo yake ni kwamba licha ya watu hao wawili kufariki dunia, majeruhi waliolazwa katika hospitali mbalimbali jijini hapa na KCMC mkoani Kilimanjaro, idadi iliyothibitishwa na polisi imefikia 60.
Habari zilieleza kuwa majeruhi wanne, hali zao zilikuwa mbaya huku mtoto, Farad Jamal (7), akiwa katika hali mbaya zaidi kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) katika Hospitali ya KCMC.
Mbowe amesema “ tukio hili ni kubwa na lina mambo mengi, chama kitawahudumia majeruhi wote.”
Kufuatia tukio hilo, msimamizi wa uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata nne, Jimbo la Arusha, Sipora Liana ambaye ni mkurugenzi wa jiji, alitangaza kuahirisha uchaguzi huo uliokuwa ufanyike juzi (Jumapili) hadi Juni 30, mwaka huu.
Liana alisema kuwa kuahirishwa kwa uchaguzi huo ni kutokana na hali tete iliyojitokeza Jumamosi na kusababisha uvunjifu wa amani hivyo kwa mtazamo huo usingeweza kufanyika kutokana na hali ya usalama kuwa mdogo.
Mkuu wa Mkoa, Mulongo alisema kuwa watu kadhaa wanashikiliwa na polisi wakihusishwa na tukio hilo na aliwasihi wananchi waendelee na shughuli zao wakati vyombo vya dola vikiendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
MAJERUHI WAZUNGUMZA
Akisimulia tukio hilo, mmoja wa majeruhi aliyelazwa katika Hospitali ya Seliani, Abdalah Alila (39) alisema kuwa akiwa katika mkutano huo majira ya saa 11.50 jioni, aliona kitu cheusi kikidondoka karibu yake na baadaye alisikia kishindo kizito.
“Ghafla nilijikuta chini na damu zikinichuruzika huku nikishindwa kutembea, nikatambaa kuomba msaada kwa watu waliokuwa wakikimbia hovyo,” alisema.
MRUSHA BOMU
Taarifa zilidai kuwa kuna mtu alionekana akirusha kitu kinachodaiwa kuwa ni bomu kwenye eneo la jukwaa karibu na gari la matangazo la chama hicho, lakini alipokuwa akifuatiliwa baada ya kutokea mlipuko huo, polisi nao walikuwa wameanza kudhibiti watu kwa kulipua mabomu ya kutoa machozi na kupiga risasi za moto, hali iliyozidisha vurugu.
Hali hiyo ilifanya barabara zote za Jiji la Arusha kujaa watu waliokuwa wakikimbia hovyo.
Kitendo cha watu kukimbia hovyo kuliwafanya polisi wengi kuingia mitaani kudhibiti watu na hivyo nao kulazimika kutumia mabomu ya machozi, hali ambayo ilizidisha taharuki.
BADO HOFU IMETANDA
Pamoja na viongozi kujitahidi kutuliza wananchi lakini bado hali ni tete jijini hapa kwa kuwa watu wana hofu hasa maeneo ambayo yana mkusanyiko wa watu wengi huku wengine wakijitahidi muda mwingi kuwa majumbani mwao.
Wananchi waliozungumza na Uwazi kwa nyakati tofauti kuhusu tukio hilo, wamemuomba Rais Kikwete kufuatilia kwa kina matukio hayo ili maswali yote yanayoulizwa hivi sasa yaweze kujibiwa japokuwa tayari amesema serikali itafanya kila liwezekanalo kuwasaka waliohusika na kitendo hicho ili washitakiwe.Chanzo:www.globalpublishers.info
Isn't the G8 supposed to alleviate global tensions? Obama and Putin put on deeply awkward show of unity after disastrous meeting at summit
President Obama and Russian leader Vladimir Putin put on an almost
comically awkward show of unity for the cameras today as they made
virtually no eye contact and grimaced as the other spoke following a
bilateral meeting at the G8 Summit.
Obama tilted his chair away from the Russian president who fidgeted with his fingers and tapped his feet.
Putin slumped down in his seat, leaned heavily on the arm rests and
stared into the distance at the scenic backdrop of Lough Erne. The
usually effusive Obama, who is never short of hugs for fellow leaders,
did not raise a smile, his shoulders hunched and jaw working hard on a
piece of gum.

Distant relations: President Obama looks grim as Russian president
Vladimir Putin stares at the floor during a bilateral press conference
at the Lough Erne resort near Enniskillen in Northern Ireland on Monday

Frosty: Obama glances away as he discusses the progress made at the
meeting between the U.S. and Russia while Putin fidgeted with his hands

Tough calls: Obama and Putin admitted that
they did not agree over the their Syrian conflict as the U.S. arms
rebel forces and Russian continues to back President Assad
The palpable tension in the room was evident after fraught discussions between the U.S. and Russia on Syria's bloody civil war.
Putin told Obama that their positions on Syria do not 'coincide' but
they conceded that they have a shared interest in stopping the violence
that has ravaged the Middle Eastern country during a two-year-old civil
war.
Obama acknowledged in the bilateral meeting that they have a 'different
perspective' on Syria but he said that both leaders wanted to address
the fierce fighting and also wanted to secure chemical weapons in the
country.
The words rang out hollowly in the press room as both leaders' body
language appeared to show that little progress had been made on the
brutal civil war which has left more than 90,000 Syrians dead.
Mtoto: Nilipigwa risasi na polisi
Arusha/Dodoma. Wakati watu waliofariki kwenye tukio la kurushwa bomu
katika mkutano wa Chadema ikifikia watatu baada ya jana kufariki kwa
mtoto Amir Ally (7), mtoto mwingine wa miaka kumi na moja aliyejeruhiwa,
amedai kwamba alipigwa risasi na polisi kwenye tukio hilo
.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe naye ametoa tamko kuwa chama chake
kina ushahidi wa kutosha wa watu waliohusika na tukio la kurushwa bomu
katika mkutano wa kampeni wa chama hicho.
Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Arusha Medical Lutheran Center (ALMC),
Dk Paul Kisanga alisema jana kuwa, Amir alifariki jana asubuhi baada ya
kupata majeraha makubwa kichwani yaliyodhuru ubongo wake.
Dk Kisanga alisema huyo ni mmoja wa watoto watano, waliojeruhiwa wakati
wakitoka madrasa huko Kaloleni, jirani na Uwanja wa Soweto kulipokuwa na
mkutano na alifariki jana asubuhi hospitalini hapo.
Alisema watoto wengine wawili ambao ni ndugu; Fatuma na Sharifa Jumanne
wamepelekwa Nairobi kwa matibabu zaidi baada ya miili yao kukutwa na
vyuma.
Dk Kisanga aliwataja watoto wengine waliojeruhiwa kuwa ni Fahad Jamal (7) ambaye yupo ICU akisubiri timu ya madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na hali yake kutoruhusu kusafirishwa. Pia yupo Abubakar Adam (11) ambaye amejeruhiwa mguuni na amelazwa katika Hospitali ya Mkoa, Mount Meru.
Dk Kisanga aliwataja watoto wengine waliojeruhiwa kuwa ni Fahad Jamal (7) ambaye yupo ICU akisubiri timu ya madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na hali yake kutoruhusu kusafirishwa. Pia yupo Abubakar Adam (11) ambaye amejeruhiwa mguuni na amelazwa katika Hospitali ya Mkoa, Mount Meru.
Mtoto aeleza kupigwa risasi
Adam alisema jana kuwa alipigwa risasi na mtu aliyekuwa amevalia sare za
polisi, wakati akitoka madrasa akiwa na ndugu yake, Fahdi katika eneo
la Soweto.
Alisema akiwa njiani, aliona watu wakimkimbiza mtu na ghafla alishangaa kupigwa risasi na kuanguka chini.
“Namkumbuka aliyenipiga risasi alikuwa amevaa sare za polisi,” alisema
Adam mwanafunzi katika Shule ya Msingi Levolosi huku akitokwa machozi.
Monday, June 17, 2013
'I'm looking for an Abraham Lincoln without the beard': Judge reveals unusual criteria for Miss USA contestants as Connecticut 25-year-old wins Donald Trump's coveted crown
By DAILY MAIL REPORTER
One of the judges of this year's Miss USA competition declared on Sunday
night that he was looking for a winner who reminded him of Abraham
Lincoln 'without the beard' before 25-year-old Connecticut beauty Erin
Brady was crowned in Donald Trump's coveted contest.
'Wait Wait ... Don't Tell Me' personality Mo Rocca offered up his
bizarre criteria as the contestants strutted their stuff in elegant
gowns and swimsuits.
Shortly after, Brady, of South Glastonbury, was announced the winner of
the beauty pageant, which took place at the Planet Hollywood
hotel-casino in Las Vegas.

Hooray: Miss Connecticut Erin Brady reacts as she is crowned by Miss USA
2012 Nana Meriwether during the Miss USA pageant at the Planet
Hollywood Resort and Casino in Las Vegas, Nevada

Winner: Miss Connecticut Erin Brady, center, beat 50 other hopefuls to win

Emotional: Miss Connecticut USA 2013 Erin Brady was overcome when she was announced as Miss USA 2013 on Sunday night
Subscribe to:
Posts (Atom)




















